Pages

Tuesday, 24 February 2015

UEFA DIMBANI TENA LEO BARCELONA UGENINI NA MAN CITY BILA YAYA MECHI NYINGINE JUVE NA DORTIMUND

Leo hii Uwanja wa Etihad Jijini Manchester utalipuka kwa mpambano mkali wa Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kati ya Manchester City na FC Barcelona.
Mechi hii ni Marudio ya Mechi ya Msimu uliopita ya Raundi hii hii ya Mashindano haya wakati Man City ilipotolewa na Barcelona kwa Jumla ya Mabao 4-1 katika Mechi mbili ambazo kila Mechi City ilimaliza Mtu 10 baada ya Mchezaji wao mmoja kupewa Kadi Nyekundu.
Katika Mechi hizo, Barcelona walishinda Mechi ya Kwanza iliyochezwa Etihad Bao 2-0 na
kwenye Marudiano huko Nou Camp, Barca ilishinda Bao 2-1.
Man City itamkosa Kiungo wao mahiri Yaya Toure ambae anamalizia Kifungo chake cha Mechi 3 alichopewa na UEFA lakini Straika wao mpya Wilfried Bony ruksa kuanza Mechi hii.
Barcelona huenda wakamchezesha Straika wao Luis Suarez ambae atakuwa akicheza Mechi yake ya kwanza Nchini England tangu aihame Liverpool mwanzoni mwa Msimu.
Akiongelea mtanange huu wa Uwanja wa Etihad, Sentahafu wa Barca, Gerard Pique, ambae aliichezea Man United ambao ni Mahasimu wakuwa wa City, alisema: “Hii ni moja ya Gemu ya Mwaka, na ni muhimu kwetu kwa sasa. Watajaribu kutushambulia na hilo linatufaa sisi. Imedhihirishwa kwamba tunakuwa vyema dhidi ya Timu zinazotushambulia kwa sababu tunaweza kupiga kaunta ataki!”
Nae Straika wa Man City, Sergio Aguero, ametamka: “Hii ni Gemu mpya na sisi sasa si sawa na Msimu uliopita na wao pia sivyo!”
Meneja wa City Manuel Pellegrini ameahidi Timu yake itacheza kwa kushambulia tu.


 MECHI NYINGINE LEO
Juventus FC vs BV Borussia Dortmund
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates