Pages

Friday, 27 February 2015

WACHEZAJI WA MBEYA CITY WALIPOKUTANA NA MEYA WA JIJI NA KUPIGA MSOSI PAMOJA

Meya wa jiji la Mbeya Mh. Athanas Kapunga amewataka wachezaji  wa Mccfc kutulia na kujipanga vizuri ili kutafuta pointi tatu muhimu kwenye mchezo ujao wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting unatarajiwa kupigwa  jumamosi hii kwenye uwanja wa Sokoine jijini hapa.
Mh Kapunga aliyasema hayo jana jioni wakati wa hafla maalum aliyoindaa kwa wachezaji hao kuwapongeza kwa namna walicheza kwa kiwango bora kwenye mchezo dhidi ya Yanga juma lililopita licha ya kupoteza mchezo huo.
“Najua mlipambana sana, dunia nzima iliona mpira mkubwa mliocheza siku hiyo licha ya kupoteza kwa sababu hata walioshinda walikiri kuwa ninyi mlikuwa bora uwanjani na hakika cha moto walikiona alisema” Mh Kapunga.
Akiendelea zaidi Mh. Kapunga alisema kuwa  baada ya kuona jinsi timu ilivyocheza siku hiyo  aliamua kuandaa hafla fupi ili kuwapongeza na kuwahakikishia kuwa licha ya kupoteza dhidi ya Yanga  lakini uongozi wa jiji bado uko pamoja nao na imani yake kubwa ni City itaibuka na ushindi jumamosi dhidi ya Ruvu Shooting.
“Tuko pamoja, uongozi wote wa jiji uko pamoja nanyi ndiyo maana jioni hii tumekutana hapa, imani yangu kubwa jumamosi tutapata  pointi tatu muhimu, naomba nikuhakikishie Mwalimu Mwambusi wewe pamoja na benchi lote la  ufundi  kuwa tunatambua kile mnachokifanya kwa ajili ya wanambeya na wapenzi wote wa timu yetu duniani kote tutaendelea kuwaunga mkono mpaka kieleweke” alisema Mh Kapunga  na kuwafanya wageni waliohudhuria kumpigia makofi mengi.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates