Pages

Saturday, 21 February 2015

WACHEZAJI WA STAND HAKUNA KUCHAT, WANYANG'ANYWA SIMU KUHOFIA KUPANGA MATOKEO NA SIMBA

Uongozi wa Stand united umeamua kuwanyang'anya simu wachezaji wake ili kuhakikisha hakuna hujuma kabla ya kuwavaa Simba kesho kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Habari za ndani kutoka Stand United zinaeleza kila mchezaji amekabidhi simu yake kwa uongozi.
“Wachezaji wametakiwa kukabidhi simu kwa uongozi na hilo limefanyika kwa ajili ya uhakika tu.
“Si kwamba Simba wametuhujumu, lakini kwa kuwa ni timu kubwa lazima tuwe makini sana katika hili,” kilieleza chanzo.
Stand itakuwa na kazi ya kuizuia Simba kesho ili angalau kukusanya pointi zitakazoikwamua eneo la mkiani.
Tayari Simba iko mjini Shinyanga tayari kwa mechi hiyo inayotarajiwa kuingiza idadi kubwa ya watu.


Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates