WINGA
wa Liverpool Philippe Coutinho ni mmoja wa Wachezaji Watano wanaochezea
Klabu za England waliotajwa kwenye Kikosi cha Timu ya Taifa ya Brazil
na Kocha Dunga ambacho kitacheza Mechi za Kirafiki baadae Mwezi huu na
France na Chile.
Coutinho aliichezea Brazil kwa mara ya kwanza Mwaka 2010 lakini baada
ya hapo hakuitwa tena hadi Mwaka Jana baada ya Kombe la Dunia
walipoadhiriwa kwao baada ya kufumuliwa Bao 7-1 na Germany kwenye Nusu
Fainali.
Msimu huu Coutinho, mwenye Miaka 22, yuko moto na Wikiendi iliyopita
ndie aliefunga Bao la ushindi murua wakati Klabu yake Liverpool
inawachapa Mabingwa wa England Man City Bao 2-1 Uwanjani Anfield.
Wachezaji wengine wanaocheza Ligi Kuu England ambao wameitwa na Kocha
Dunga ni Kiungo wa Man City Fernandinho pamoja na Wachezaji Watatu wa
Chelsea Oscar, Willian na Filipe Luis.
Wachezaji waliorudishwa tena Kikosini ni Robinho, anaechezea Santos huko Brazil, na Marcelo wa Real Madrid.
Brazil itacheza na France ndani ya Stade de France Mjini Paris hapo
Machi 26 na Machi 29 kucheza na Chile kwenye Uwanja wa Arsenal, Emirates
Stadium, Jijini London.
KIKOSI KAMILI:
Makipa: Jefferson, Diego Alves, Marcelo Groeh
Mabeki: David Luiz, Marquinhos, Thiago Silva, Miranda, Filipe Luis, Danilo, Fabinho, Marcelo.
Viungo: Luiz Gustavo, Fernandinho, Elias, Souza, Oscar, Willian, Douglas Costa, Philippe Coutinho.
Mafowadi: Neymar, Robinho, Roberto Firmino, Diego Tardelli.
Friday, 6 March 2015
Home »
» ANGALIA KIKOSI CHA BRAZIL KITAKACHOCHEZA NA CHILE MWEZI HUU COUTHINO,ROBHINO NA MARCELO WARUDISHWA KIKOSINI
0 comments:
Post a Comment