Pages

Friday, 6 March 2015

COUTIHNO: "NAUMIA SANA KUIKOSA MECHI YA SIMBA"

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Andrey Coutinho, juzi Jumatano alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga chozi mara baada ya kupewa taarifa ya kuikosa mechi dhidi ya Simba.
Mbrazili huyo alifanyiwa vipimo kwenye Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam na baada ya hapo ndipo akapewa taarifa hizo ambapo anasumbuliwa na maumivu ya goti aliyopata wakati timu hiyo ilipovaa na Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Prisons.
Coutinho alisema kuwa bora angekosa mechi zote lakini siyo dhidi ya Simba yenye upinzani mkubwa.
“Ninaumia sana kuikosa mechi dhidi ya Simba, kauli iliyotolewa na madaktari leo (Jumatano) mara baada ya kufanyiwa vipimo imenifanya nikose furaha,” alisema Coutinho.
Aidha, Coutinho aliongeza kuwa, anaamini kikosi chake kipo fiti na wachezaji wenzake lazima watawafunga Simba kutokana na jinsi walivyo fiti kwa sasa.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates