VINARA wa Ligi Kuu England Chelsea jana nusura wakose ushindi ugenini na Hull City baada ya kuongoza 2-0 na kuiruhusu Hull kusawazisha na Gemu kuwa 2-2 lakini Loic Remy alitoka Benchi na kuja kuwapa ushindi wa Bao 3-2.
Ushindi huu umeifanya Chelsea izidi kuongoza Ligi ikiwa Pointi 6 mbele ya Mabingwa Watetezi Man City lakini pia Chelsea wana Mechi 1 mkononi.
************,*********************
LIGI KUU ENGLAND
Msimamo-Timu za Juu
1. Chelsea Mechi 29 Pointi 67
2. Man City Mechi 30 Pointi 61
3. Arsenal Mechi 30 Pointi 60
4. Man United Mechi 30 Pointi 59
5. Liverpool Mechi 30 Pointi 59
************************************
Katika Mechi hiyo Bao za Chelsea zilifungwa na Eden Hazard Dakika ya 2 na DiegobCosta Dakika ya 9 huku Hull wakifunga Dakika za 26 na 28 kupitia Ahmed El Mohamady na Hernandez.
Bao la ushindi la Chelsea lilifungwa na Loic Remy alieingizwa kumbadili Diego Costa na kupachika Bao lake Dakika ya 77.
Kwenye Mechi nyingine ya Ligi Kuu England iliyochezwa huko Loftus Road Everton iliichapa QPR Bao 2-1.
Bao za Everton zilufungwa Dakika za 18 na 77 na Seamus Coleman na Aaron Lennon likiwa Bao lake la kwanza kwa Everton tangu atue hapo kutoka Spurs.
0 comments:
Post a Comment