BARCELONA wamepaa Pointi 4 mbele kileleni mwa La Liga baada ya ushindi wa 2-1 kwenye El Clasico dhidi ya Mahasimu wao wakubwa Real Madid kwenye Mechi iliyofanyika Nou Camp Jana Usiku.
Barca ndio waliotangulia kufunga katika Dakika ya 19 kwa Goli la Kichwa la Jeremy Mathieu alipounganisha Krosi ya Lionel Messi.
Real walisawazisha Dakika ya 31 baada ya Karim Benzema kumpa pasi ya kisigino Cristiano Ronaldo aliemchambua Kipa Bravo na kutikisa nyavu.
Hadi Mapumziko, Barca 1 Real 1.
Kipindi cha Pili Dakika ya 56, Dani Alves alipiga pasi ndefu na ya juu ya Mabeki wa Real, Pepe na Sergio Ramos, na kunaswa vyema na Luis Suarez aliemalizia vyema na kuipa Barca Bao la Pili na la ushindi.
0 comments:
Post a Comment