Mlinzi wa kutumainiwa wa City Juma Nyosso anatarajia kurejea uwanjani kutumikia timu yake kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara dhidi ya Azam Fc uliopangwa kuchezwa Chamanzi Complex mapema mwezi ujao.
Nyosso aliyekuwa akitumikia adhabu ya kufungiwa michezo 8 atakamilisha kifungo hicho jumamosi ya tarehe 4.4 2015 wakati City itakapokuwa uwanjani kucheza na Ndanda Fc kwenye mchezo mwingine wa ligi hiyo utakaochezwa kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoni Mtwara.
![]() |
JUMA NYOSSO WA PILI KUTOKA KUSHOTO |
Akizungumza mapema leo Katibu Mkuu City Emmanuel Kimbe amesema kurejea kundini kwa Nyosso kutaongeza nguvu kubwa kikosini hasa kwenye wakati huu ambao timu inafanya jitihada za dhati kupata matokeo ili kusaka nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi.
“Kila mmoja hapa anayo kumbukumbu ya kazi nzuri aliyoifanya Nyosso kwenye mechi alizocheza kabla ya kupata adhabu, niseme wazi kuwa ni mchezaji muhimu ambaye uwepo wake unaongeza kitu, kila mmoja anaweza kuitafsiri adhabu ile kwa namna yake, lakini uwanjani kuna mambo mengi, kuna wakati unaweza kufanya jambo usijue ulilifanya vipi, kizuri kwetu ni kuwa anamaliza adhabu hiyo na kurudi kuitumikia timu” alisema.
Wakati huo huo nyota wanaunda safu ya ushambuliaji Paul Nonga, Mwegane Yeya na Themi Felix wamesema wako tayari kuwasha moto ndani ya uwanja wa Nangwanda sijaona kwa lengo moja tu la kuipatia City ushindi kwenye mchezo dhidi ya ndanda fc.
0 comments:
Post a Comment