Pages

Monday, 23 March 2015

YANGA YABAKIZA MECHI 8 MICHEZO SABA MFULULIZO WATACHEZA NYUMBANI

Baada ya juzi Jumamosi kufanikiwa kuifunga Mgambo JKT mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, sasa vinara wa Ligi Kuu Bara, Yanga, wamebakiza mchezo mmoja tu ambao ni sawa na dakika tisini, nje ya Jiji la Dar.


Yanga wamejikusanyia pointi 37 kwa kucheza michezo 18, wamebakiza michezo nane tu ili kuhitimisha ligi hiyo msimu huu ambayo inatarajiwa kufikia tamati Mei 9, mwaka huu.

Katika michezo hiyo nane, Yanga itacheza michezo saba mfululizo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar ambao wanautumia kwa michezo yao ya nyumbani huku ule wa mwisho wakilazimika kusafiri mpaka mkoani Mtwara kupambana na Ndanda FC kwenye Dimba la Nangwanda Sijaona.

Wakati Yanga ikiwa imebakiza mchezo mmoja ugenini, wapinzani wao wanaowafuatia kwa karibu, Azam nao pia wamebakiza mchezo mmoja dhidi ya Mtibwa Sugar huku Simba wao wakiwa wamebakiza michezo miwili ambapo watacheza dhidi ya Kagera na Mbeya City.

Yanga na Azam zina nafasi kubwa ya kulitwaa kombe hilo endapo tu zitatumia vizuri mechi hizo za nyumbani.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates