Pages

Sunday, 1 March 2015

KILI MARATHON WANARIADHA WAKENYA WAFUNIKA, MTANZANIA ASHIKA NAFASI YA KWANZA FULL MARATHON

Mashindano ya riadha ya Kili maarufu kama Kili marathon yamemalizika jana huku wakenya wkiendelea kuwapoteza watanzania katika mbio hizo
Mbio hizo zilishuhudia mwanariadha wa Tanzania Fabiola William (32),ameibuka mshindi wa kilomita 42 (Full Marathon) katika mbio za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika jana mjini hapa na kujinyakulia Sh milioni 4 baada ya kutumia 2:49:51.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na Rosaline David (Kenya) aliyetumia 2:50:39 na kujinyakulia Sh milioni mbili wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na Joan Cherop (Kenya) alitumia 2:50:44 na kujinyakulia Sh milioni moja.

Kwa upande wa Half Marathon Kiloimita 21 wanaume,  Ismael Juma (Tanzania), aliibuka mshindi baada ya kutumia 1:03:05 na kujinyakulia Sh milioni 2 huku nafasi ya pili ikienda kwa Emmanuel Giniki (Tanzania), aliyetumia 1:03:15 na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Theotil Joseph (Tanzania), aliyetumia 1:03:25.
Akizungumza katika mbio hizo, mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe,  aliwapongeza waandaaji wa tukio hilo la aina yake.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates