Pages

Friday, 27 February 2015

BOMU LA VITA KUU YA PILI YA DUNIA LAGUNDULIKA KWENYE UWANJA WA BORUSSIA DORTMUND

Huko Ujerumani zipo habari kuwa Uwanja wa Signal Iduna Park na Maeneo ya jirani yalilazimika kuondolewa Watu baada ya kugundulika Bomu ambalo halijalipuka.
Bomu hilo lenye uzito wa Ratili 550 inasemekana ni la asili ya Uingereza na Maafisa walikuwa wakiendelea kujaribu kulitegua.
Ugunduzi wa Bomu hilo ulisababisha Mkutano na Wanahabari wa Kocha wa Borussia Dortmund, Jurgen Klopp, kuhusu Dabi yao ya Jumamosi dhidi ya Schalke kuahirishwa.
Huko Germany kugundulika kwa Mabomu ambayo hayajalipuka kutoka Vita Kuu ya Pili Duniani iliyopiganwa kuanzia Mwaka 1939 hadi 1945 ni kitu cha kawaida kwani Nchi hiyo iliyokuwa ikitawaliwa na Fashisti Hitler ilikuwa ikivurumishwa na Mabomu kutoka kwa Uingereza na Washirika wake pamoja na Urusi.
Kwenye Vita hvyo, Mji wa Dortmund uliharibiwa vibaya kwa kuangushiwa Mabomu kutoka kwenye Ndege za Kivita.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates