Kipa wa yanga Ally Mustapha Bathez amefikisha dakika 608 katika michezo ya ligi kuu ya vodacom kabla ya kuruhusu goli katika nyavu zake, ambapo aliruhusu katika mchezo wa jana katika dakika ya 68 goli likifungwa na Peter Mapunda.
Bathez amecheza jumla ya dakika 716 katika michuano yote bila kuruhusu nyavu zake kuguswa, ambapo mara ya mwisho alifungwa na Amur Omry Janja katika michuano ya kombe la mapinduzi katika dakika ya 72.
Bathez vile vile alisimama langoni pale yanga walipo wakabili BDF XI ya Botswana katika kombe la shirikisho ambapo alimaliza dakika 90 bila ya nyavu zao kuguswa.
Bathez ameanza kuidakia yanga katika msimu huu katika michuano ya Mapinduzi, kabla ya hapo alikuwa anadaka Deo Munish Dida.
Monday, 23 February 2015
Home »
» HII HAPA REKODI YA KIPA WA YANGA ALLY MUSTAPHA 'BARTEZ" USIMPIME!
0 comments:
Post a Comment