Rais wa Shrikisho la Mpira wa Miguu nchini –TFF Bw Jamal Malinzi ametuma salama za pongezi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Ufukweni (Beach Soccer), Bw. Ahmed Mgoyi kwa ushindi wa jumla wa mabao 12- 9 dhidi ya timu ya Taifa kutoka nchini Kenya.
Timu ya Taifa ya Tanzania ya Sola la Ufukweni, mwishoni mwa wiki iliibuka na ushindi wa mabao 7-6 katika mchezo uliofanyika kwenye Ufukwe wa klabu ya Escape 1 eneo la Msasani Jijini Dar es salaam.
Katika salamu zake Bw. Malinzi amesema ushindi walioupata timu ya soka la Ufukweni mwishoni mwa wiki, umeitangaza vizuri nchi ya Tanzania na kuwataka Viongozi wa soka la Ufukweni, makocha, wachezaji kutobweteka na ushndi huo, zaidi kujipanga kwa maandalizi ya mchezo utakaofuata.
0 comments:
Post a Comment