LIGI KUU VODACOM Leo hii inaendelea kwa Mechi 3 lakini Vigogo wa Soka wapo dimbani Jumapili ambapo Yanga, Simba na Azam FC watacheza Mechi zao.
Hii Leo Kagera Sugar wapo huko ‘kwao’ Kambarage Mjini Shinyanga kucheza na Polisi Moro, Ndanda FC wapo Nyumbani Nangwanda, Mtwara kucheza na Coastal Union wakati Mgambo JKT wako Mkwakwani Mjini Tanga kuikarbisha Mtibwa Sugar.
Jumapili ndiyo Siku ya Vigogo wakati Yanga, ambao wanaongoza Ligi wakiwa Pointi 2 mbele ya Mabingwa Watetezi Azam FC, wako huko Sokoine Mjini Mbeya kucheza na Watoto wa Nyumbani, Mbeya City.
Pia Jumapili Simba wako Ugenini huko Shinyanga kucheza na Stand United na Azam FC wako kwao Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kucheza na Tanzania Prisons.
0 comments:
Post a Comment