Pages

Saturday, 21 February 2015

LIGI KUU VODACOM- NDANDA YAIUA COAST NYUMBANI VIWANJA 3 MECHI 3 MAGOLI 3 KESHO SIMBA, YANGA,AZAM ZOTE DIMBANI

Hii Leo wakicheza nyumbani Ndanda FC wameutumia vyema uwanja wao wa nyumbani Nangwanda baada ya kuitandika Coastal Union ya tanga goli 1-0 katika mchezo ulioonekana kuwa mgumu kwani hadi mapumziko kila timu haikuona labgo la mwenzie
Goli pekee la ndanda limefungwa kipindi cha pili dk ya 73
 Kagera Sugar wakiwa Kambarage Mjini Shinyanga wamepata ushindi wa goli moja dhidi ya Polisi Moro wakati Mgambo JKT wakiwa Mkwakwani Mjini Tanga wameitandika  Mtibwa Sugar goli 1-0
Jumapili ndiyo Siku ya Vigogo wakati Yanga, ambao wanaongoza Ligi wakiwa Pointi 2 mbele ya Mabingwa Watetezi Azam FC, wako huko Sokoine Mjini Mbeya kucheza na Watoto wa Nyumbani, Mbeya City.
Pia Jumapili Simba wako Ugenini huko Shinyanga kucheza na Stand United na Azam FC wako kwao Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kucheza na Tanzania Prisons.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates