Wanachama na viongozi wa Klabu ya Simba, wanatarajia kukutana kesho Jumapili saa nne asubuhi katika mkutano mkuu utakaofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi Oysterbay jijini Dar ili kuweka mambo sawa.
Rais wa Simba, Evans Aveva,akizungumza na INFO RADIO amefunguka kuwa, ajenda watakayokwenda kuijadili katika mkutano huo ni kuhusu mwenendo wa timu hiyo katika ligi kwa lengo la kuikwamua timu ili iwe na kiwango kizuri katika mechi zinazofuata.
Alisema mkutano huo utakuwa wa kawaida na watahakikisha wanatoa nafasi kwa kila mtu kutoa ya moyoni kwa lengo la kujenga.







0 comments:
Post a Comment