Timu ya Taifa ya Tanzania ya Soka la Ufukweni (Beach Soccer) kesho
jumamosi itacheza mchezo wa marudiano dhidi ya timu ya Taifa ya Kenya, mchezo
utakaoanza majira ya saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Escape One Club Msasani
jijini Dar es salaam.
Wageni timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni kutoka nchini Kenya
wanatarajia kuwasili leo jioni jijini Dar es salaam, tayari kabisa kwa ajili ya
mchezo huo wa marudiano siku ya jumamosi
Katika mchezo wa awali uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini
Mombasa, timu ya Taifa ya Tanzania iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 5 – 3
dhidi ya wenyeji timu ya Taifa ya Kenya na kujitengenezea mazingira mazuri ya
kusonga mbele katika hatua inayofuata.
0 comments:
Post a Comment