Pages

Wednesday, 25 February 2015

WACHEZAJI TEGMEO WA MTIBWA SUGAR HAWANA MPANGO TENA NA TIMU HIYO WAGOMA KUONGEZA MIKATABA

Wachezaji watano wa Mtibwa Sugar, tena wale muhimu, mikataba yao imefikia tamati na wamegoma kuongeza mipya!

Nyota wanaotajwa kutangaza nia ya kuondoka ni kipa tegemeo Said Mohammed, Salim Mbonde na Henry Joseph Shindika, ambaye alisaini miezi sita katikati ya msimu huu baada ya kuachana na Simba mwishoni mwa msimu uliopita.

Habari za kina zinasema kuwa, Mohammed yupo mguu ndani-nje kujiunga na mabingwa watetezi, Azam, Mbonde anawindwa na Simba huku Shindika yeye akifunguka mwenyewe kuwa kwa sasa hawezi kuongeza mkataba mwingine hadi msimu umalizike huku akikaribisha timu yoyote.

“Mkataba wangu unaisha na bado sijafanya mazungumzo na mtu yeyote mpaka sasa, hata hivyo sipo tayari kwa kipindi hiki. Nasikilizia kwanza upepo wa dili kwenye usajili, unajua unaweza kupata dili la maana kwenye kipindi cha usajili. Iwapo kutakuwa na timu inanitaka, basi niko tayari kuisikiliza hata sasa hivi,” alisema nyota huyo wa zamani wa Simba na Taifa Stars.

Msemaji wa Mtibwa, Thobias Kifaru, alikiri kuwepo kwa dalili za nyota wao kutaka kuondoka lakini akasema watakaa chini kuzungumza nao.

Timu hiyo imeambualia pointi moja katika mechi tano za hivi karibuni na kushushwa kutoka kileleni hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi kuu, ambayo inaongozwa na mabingwa wa kihistoria, Yanga.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates