Pages

Wednesday, 4 March 2015

KUELEKEA MECHI YA WATANI SIMBA YAKATAA MECHI YA KIRAFIKI ZANZIBAR


Kocha wa Simba, Goran Kopunovic amekataa kikosi chake kucheza mechi ya kirafiki usiku.
Wanachama wa Simba walio Zanzibar walikuwa wametafuta mechi ya kirafiki baada ya ombi la kocha huyo lakini ikaonekana inatakiwa kuchezwa usiku.
Kopunovic amechukua uamuzi wa mechi hiyo kwa kusema wao na Yanga Jumapili watacheza jioni, hivyo asingependa kikosi chake kucheza mechi jioni.
"Hauwezi kucheza mechi ya kirafiki usiku halafu ucheze mechi unayojiandaa jioni. Katika uchezaji suala la mazingira pia ni muhimu sana," alisema Kopunovic.
Kocha huyo Mserbia amekuwa akiendelea na mazoezi huku akisaidiana na msaidizi wake, Selemani Matola wakijiwinda kutaka kuitwanga Yanga katika mechi ya Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates