Pages

Sunday, 8 March 2015

OKWI AISAIDIA SIMBA YAIUA YANGA 1-0 NDANDAHOI TANGA WAPIGWA 3-1 NA MGAMBO, MTIBWA NA MBEYA CITY HAKUNA MBABE


Mshambuliaji wa kimataifa Emmanuel Okwi, Leo hii amerudisha furaha ya mashabiki wa   Simba baada ya kufunga Bao pekee na la ushindi walipoilaza Yanga Bao 1-0 kwenye Mechi ya Ligi  Kuu Vodacom.
Bao hilo la Okwi lilifungwa Dakika ya 53 na kuipandisha Simba hadi Nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 26 kwa Mechi 17 na juu yao wapo Mabingwa Watetezi Azam FC wenye Pointi 30 kwa Mechi 16 na Yanga bado wapo kileleni wakiwa na Pointi 31 kwa Mechi 16.
Yanga walimaliza Mechi hii wakibaki Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Haruna Niyonzima kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu karibuni na mwisho.
Yanga na Simba zimekutana mara 103, kati ya hizo, Yanga ilishinda 38, Simba 32,huku mara 33 zikitoka sare.
Nao ndanda wakicheza ugenini jijini tanga wamekubali kipigo cha magoli 3 kwa 1  kutoka mgambo Jkt magoli ya mgambo yamefungwa na Salim Aziz Gilla aliyefunga magoli mawili dakika ya  12na 70 huku lingine likifungwa na Malimi Busungu dk 26 goli pekee la Ndanda Gideon Benson dk 45
Huko Manungu Mtibwa sugar wametoka sare ya goli 1-1 dhidi ya Mbeya city goli la Mtibwa limefungwa kwa kichwa dk 14 na Musa hasani mgosi akiunganisha mpira wa adhabu  uliopigwa na na goli la mbeya city limefungwa na themi felix

Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates