Pages

Wednesday, 4 March 2015

YANGA KUTISHIA KUGOMEA MECHI NI MKWARA TU TAARIFA WANAYO KWA MUJIBU WA BODI YA LIGI

Wawakilishi wa Tanzania katika kombe la shirikisho Yanga wametangaza nia ya kugomea mchezo dhidi ya ligi kuu ya vodacom dhidi ya JKT Ruvu ulipangwa kuchezwa marchi 11 mwaka huu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Mkuu wa kitengo cha habari wa yanga Jerry Muro, akizungumzaq na vyombo vya habari leo amesema kuwa yanga hawataingiza timu uwanjani marchi 11, kama mchezo huo hauto chezwa kesho, kama ratiba ya awali ilivyokuwa inaonyesha.

Jerry alisema kuwa mabadiliko hayo ya ratiba uongozi wa yanga hawaya jui kwa kuwa hawana taarifa maalum toka kwa bodi ya ligi juu ya mabadiliko hayo ya ratiba.
Muro amesema bodi ya ligi imeonyesha kwamba haitaki Yanga ifanikiwe katika kampeni zao za kombe la Shirikisho kwa kuitaka kuucheza mchezo huo Machi 11 ikiwa ni siku tatu kabla ya kushuka katika Uwanja wa Taifa kucheza na Plutinum ya Zimbabwe.
"Tumewaambia tangu jana kama wameufuta mchezo wa kesho na badala yake wakaupeleka Machi 11 Yanga hatutakuja uwanjani kwakuwa huo sio uzalendo hatuwezi kuacha maandalizi ya mechi yetu ya kimataifa kuangalia mechi ya ligi." aliongeza Muro

Wakati Muro akisema hayo kaimu ofisa mtandaji Mkuu wa bodi ya ligi Fatma Abdallah amesema kuwa yanga walitumia kwa njia ya Email mabadiliko hayo ya ratiba, toka februari 15 mwaka huu. Fatma Abdallah alisema hayo pale alipo kuwa anahojiwa na kituo cha redio nchini. 
Mabadiliko ya ratiba msimu huu wa ligi kuu ya vodacom yamekuwa yakitokea mara kwa mara, na kupelekea kuharibu mipango ya timu shiriki kutokana na mabadiliko hayo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

IDADI YA WANAOTEMBELEA BLOG HII

Blog Archive

Recent Posts

Fashion

3/Fashion/big-col-right

Recent Posts

Header Ads

Followers

Powered By Blogger

Tags

Maoni

3/recent-comments

WASILIANA NASI

Popular Posts

Labels

Blog Archive

Blogger templates