Ligi kuu ya hispania iliendelea jana kwa michezo minnne
Wakicheza Ugenini na Sevilla ambayo haijafungwa kwao katika Mechi 31, Barcelona Jana waligundua ugumu wa hilo baada ya kutangulia 2-0 na kujikuta wakitoka Sare 2-2 katika Mechi ya La Liga.
Sare hii imewafanya Barca waongoze La Liga kwa Pointi 2 tu mbele ya Real Madrid ambao Jana waliichapa Eibar 2-0.
Jana Barca walitangulia kwa Bao za Lionel Messi na Neymar za Dakika za 14 na 31 na Seville kurudisha katika Dakika za 38 na 84 kwa Bao za Ever Banega na Kevin Ganeiro.
*********************
Bao za Cristiano Ronaldo, Javier Hernandez 'Chicharito' na Jesse Rodriguez zimewapa ushindi wa Bao 3-0 Real Madrid walipocheza kwao Santiago
Bernabeu na Eibar katika Mechi ya La Liga.
Ushindi huu umeisogeza Real kuwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Barcelona ambao wametoa sare ya 2-2 na Timu ngumu Sevilla isiyofungika kwao.
*********************
MATOKEO YA MECHI ZOTE
Jumamosi Aprili 11
Real Madrid CF 3 SD Eibar 0
Malaga CF 2 Atletico de Madrid 2
Sevilla FC 2 FC Barcelona 2
Celta de Vigo 6 Rayo Vallecano 1
UD Almeria 3 Granada CF 0
*****************
MICHEZO YA LEO
Jumapili Aprili 12
1300 Getafe CF v Villarreal CF
1800 RCD Espanyol v Athletic de Bilba
2000 Real Sociedad v Deportivo La Coruna
2200 Cordoba CF v Elche CF
*************
2130 Jumatatu Aprili 13
Valencia C.F v Levante
0 comments:
Post a Comment