Jumapil Vigogo wa Spain, Barcelona na Real Madrid, watavaana huko Nou Camp kwenye Mechi ya La Liga ambayo hubatizwa Jina la El Cladico na ambayo safari hii itakwenda mbali kutoa fununu ya Ubingwa na pia nania atazoa Pichichi.
Mechi hii inazikutanisha Barca wanaongoza La Liga wakiwa Pointi 1 mbele ya Real huku zote zimecheza Mechi 27 na kubakiza 11.
****************************
EL CLASICO- Uso kwa Uso:
-Barcelona ushindi 89
-Real Madrid ushindi 92
-Sare 48
*****************************
Katika Mechi yao ya kwanza Msimu huu, Real waliichapa Barca Bao 3-1 huko Santiago Bernabeu na tangu wakati huo hadi hivi karibuni walikuwa Vinara wa La Liga.
Lakini baada ya kukumbwa na Majeruhi na hasa kuumia kwa Beki Sergio Ramos na Viungo Luka Modric na James Rodriguez, Real wakaanza kupoteza mwelekeo na kushinda Mechi 3 tu kati ya 6.
Hapo ndipo Barca wakapata mwanya na kuitoa Real kileleni na wao sasa kuongoza Ligi wakiwa Pointi 1 Juu ya Real.
************************************
La Liga
Msimamo Timu za Juu
1. Barcelona Mechi 27 Pointi 65
2. Real Madrid Mechi 27 Pointi 64
3. Valencia Mechi 28 Pointi 60
5. Atletico Mechi 27 Pointi 55
************************************
Mbali ya sakata la mbio za Ubingwa kati ya Barca na Real pia zipo mbio za Pichichi, Tuzo ya Ufungaji Bora La Liga kati ya Mastaa wa Timu hizo, Lionel Messi wa Barca na Cristiano Ronaldo wa Real.
Hadi sasa Messi anaongoza akiwa na Bao 32 na Ronaldo ana Bao 30.
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
BARCELONA (Mfumo 4-3-3):
-Bravo
-Alves, Pique, Mathieu, Alba
-Mascherano, Rakitic, Iniesta
-Messi, Suarez, Neymar
REAL MADRID (Mfumo 4-1-4-1):
-Casillas
-Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo
-Kroos
-Bale, Modric, Isco, Ronaldo
-Benzema
source; soka in tanzania